TUMIA BIDHAA BORA ZA AZAM BAKHRESA

Kampuni Ya H&M Yaomba Radhi Juu Ya Picha Ya Kibaguzi


Kampuni ya mavazi ya H&M imeomba radhi kufutia picha ya tangazo la nguo kutafsiriwa kuwa la kibaguzi kwa mtu mweusi.

Barua ya kuomba radhi imeelezea kuwa kampuni  hawakuwa na nia mbaya kama ilivyo tafsiriwa na baadhi ya watu baada ya kijana huyo kuvaa T-Shirt iliyoandikwa “ Coolest Monkey In The Jungle” hata hivyo imesema kuwa watafanya uchunguzi kuhusu mtu aliye husika katika kuchapisha nguo hiyo.
Kutokana na Tatizo hili limepelekea Kampuni hiyo kmpoteza msanii The Weeknd ambaye alikuwa na ubia nao toka September,The Weeknd ameandika katika account yake ya Twitter,"woke up this morning shocked and embarrassed by this photo. i’m deeply offended and will not be working with @hm anymore..."  


EmoticonEmoticon