TUMIA BIDHAA BORA ZA AZAM BAKHRESA

R.I.P | Agness Masogange Afariki Dunia

Video Queen maarufu nchini Tanzania, Agness Gerald maarufu kama Masogange amefariki dunia jioni ya leo Aprili 20, 2018 katika hospitali ya Mama Ngoma iliyopo Mwenge, jijini Dar es salaam.
Kifo chake kimeelezwa kwamba kikubwa kilichosababisha ni Tatizo La Pumu alilokuwa nalo linamsumbua na lingine ikiwa ni upungufu wa damu pia.
Mwili wa Agness Masogange tayari umeshawasili katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam kwa ajili ya kuhifadhiwa kabla ya kutangazwa kwa ratiba za mazishi.
Wiki tatu zilizopita marehemu alishindwa kuhudhuria mahakamani kusikiliza kesi iliyokuwa ikimkabili kwa kulazwa hospitalini, hii ni kabla ya kesi hiyo kutolewa hukumu wiki iliyopita.
Agness amepata umaarufu baada ya kuonekana kwenye video ya Bell 9 inayoitwa Masogange.

TUNATOA POLE KWA NDUGU NA JAMAA WALIOFIKWA NA MSIBA.

R.I.P AGNESS


EmoticonEmoticon