TUMIA BIDHAA BORA ZA AZAM BAKHRESA

RASMI;Zari Ameamua Kuachana Na Diamond Platnumz Siku Ya Wapendanao.Alichokiandika Zari Mwenyewe

Sad News/Good News ("Siku zari anasema ananiacha,nitatambaa na Magoti hapa mpaka South Africa Nikimlilia...." 

Baada ya headlines za muda mrefu na mfululizo wa tetesi za penzi la Zari na muimbaji wa Bongofleva Diamond Platnumz kudaiwa kuyumba, hatimae leo Zari ameamua kuwatangazia mashabiki wake kuwa ameamua kuachana na Diamond Platnumz kwa madai ya mfululizo wa matukio ya usaliti wa kimapenzi.
Zari ametangaza kuachana na Diamond Platnumz kupitia ukurasa wake wa instagram na ameandika ujumbe mrefu ulioeleza sababu zote zilizomfanya kufikia maamuzi hayo licha ya kuwa yeye na Diamond wamezaa watoto wawili Nillan na Tiffah, kupitia ukurasa wake wa instagram Zari ameandika hivi.
Elewa kuwa hiki ni kitu kigumu sana kwangu kukifanya, kumekuwa na tetesi mbalimbali baadhi kati ya hizo zimekuwa na ushaidi ambao umekuwa ukisambaa katika vyombo vya habari kuhusiana na usaliti wa kimapenzi unaofanywa na Diamond, kwa huzuni nimeamua kuvunja uhusiano wangu wa kimapenzi na Diamond kwa heshima yangu,Tunaachana kama wapenzi lakini sio kama wazazi hii hainipunguzii mimi kuwa mtu wa kujitegemea, mama mwenye kujali na Boss Lady, wote mnatakiwa kufahamu hilo nitaendelea kujijenga kama mwanamke mwenye ushawishi, nitawaamasisha wanawake wote kuwa maboss Ladies,Nitawafundisha watoto wangu wanne wa kiume kuwaheshimu wanawake na nitamfundisha binti yangu ni nini maana ya heshima, nimekuwa katika kiwanda cha burudani kwa miaka 12 sasa pamoja na changamoto zote hizo lakini nimefanikiwa kuwa mshindi kwa sababu mimi ni mshindi nawatakiwa wote siku njema ya wapendanao
Understand that this is very difficult for me to do. There have been multiple rumors some with evidence floating around in ALL SORTS of media in regards to Diamond’s constant cheating and sadly I have decided to end my relationship with Diamond, as my RESPECT, INTEGRITY, DIGNITY & WELL BEING cannot be compromised. We are separating as partners but not as parents. This doesn’t reduce me as a self-made individual, and as a caring mother, and the boss lady you have all come to know. I will continue to build as a mogul, i will inspire the world of women to become boss ladies too. I will teach my four sons to always respect women, and teach my daughter what self-respect means. Unlike many, I’ve been in the entertainment industry for 12 years, and through all my challenges I came out a victor because I am a winner, and so are all of you Zari supporters. HAPPY VALENTINE'S
A post shared by Zari (@zarithebosslady) on

Mpaka sikukuu ya Wapendanao inaisha na kuingia siku nyingine,Diamond alikuwa hajaandika chochote katika page yake ya Instagram zaidi ya kusheherekea ushindi wa tuzo ya Soundcity ambayo ametumiwa Tanzania cs wakati wa ugawaji wa Tuzo hiyo hakuweza kufika. 


EmoticonEmoticon